Thursday 29 May 2014

KUHUSU HANANG


Ramani ya mkoa wa Manyara
Hanang ni moja kati ya wilaya tano zilizopo katika mkoa wa manyara nchini Tanzania. Ipo umbali wa kilomita 242 kusini magharibi mwa Arusha, na km 197 kwa kipimo cha anga (Flight Distance). Kwa upande wa kaskazini imepakana na wilaya ya Mbulu na Babati, kusini mashariki ni mkoa wa Dodoma, na kusini magharibi ni mkoa wa Singida. Kulingana na sensa ya mwaka 2012 wilaya ya hanang ilikuwa na jumla ya watu 275,990.

Wilaya ya hanang imegawanywa katika kata 25 ambazo ni:

·   Balangdalalu
  • Bassodesh
  • Bassotu
  • Dirma
  • Endasak
  • Endasiwold
  • Ganana
  • Gehandu
  • Gendabi
  • Getanuwas
  • Gidahababieg
  • Gisambalang
  • Gitting
  • Hidet
  • Hirbadaw
  • Katesh
  • Lalaji
  • Laghanga
  • Masakta
  • Masqaroda
  • Measkron
  • Mogitu
  • Nangwa
  • Simbay na
  • Sirop

Watu na style za maisha
Ramani ya Wilaya ya Hanang

Wilaya ya Hanang imekaliwa na makabila makubwa mawili ambayo ni Wairaqw na Wabarbaig. Wabarabaig wamekuwa kivutio kikubwa sana cha watalii wa nje kutokana na tamaduni zao ambazo hazijaathiriwa sana na tamaduni za kimagharibi. Wageni wamekuwa wakivutiwa sana na mavazi ya asili ya ngozi kwa wanawake na mashuka mekundu maarufu kama migorori iliyotengenezwa kwa ustadi wa hali ya juu na kupambwa na shanga za rangi mbambali na vifungo vilivyoshonwa kwa ufundi na kuwekwa marinda maarufu kama “sapsapt”

Wageni wako huru kujichanganya na makabila haya na kupokelewa kwa ukarimu kama ilivyo asili ya makabila haya.


Kama unapeda ndege Hanang ndo sehemu ya kuwaona kwani kuna zaidi spishi 400 za ndege watakaokusindikiza kwa nyimbo kipindi chote utakapokua unatembelea maeneo tofauti ya wilaya hii. 

No comments:

Post a Comment