Saturday 14 June 2014

Mount Hanang, People and lifestyle.

About Hanang Mountain
Hanang District is situated in Manyara region, about 242 km south west of Arusha. Mount Hanang, standing at 3418m, is the fourth highest mountain in Tanzania and a dominant landmark in Hanang district. . The spectacular views of small craters, Lake Bakangida, The Mangati plains stretching at the south and the Rift Valley escarpment at the North West.
 
Hanang People
This district is inhabited by the two major ethnic groups, namely the Barbaig and the Iraqw. Visitors can mix freely with the Barbaig, commonly known as the Mang’ati living in the Mang’ati plains. If you are interested in bird watching, 400 bird species will welcome you on your walks in the area. The Barbaig are ethnically classified as Nilotes where as the Iraqw are referred to as southern Cushites.Both of them have rich and interesting culture. The Barbaig women are usually clad in goatskin skirts and cotton blanket. Men are usually dressed in black cloth, and they walk about carrying spears. The Iraqw people are usually attire in colorful cotton blankets. The main economic activities in Hanang district is subsistence and commercial farming. This is predominantly practiced by the Iraqw. The Barbaigs are predominantly pastoralists. The Iraqw also keep livestock though they are not highly dependent on them as the Barbaigs.
 

The people of Hanang offer:
• A special Barbaig cultural insight hike
• An exclusive Mount Hanang climb
• Cycling expeditions through remote areas
• A chance to participate in local brick and pottery making and beer brewing

Guides: English speaking guides who know the area will help you around. A Barbaig born guide will tell you about Barbaig culture.

Hanang Climbing Route

The easiest way to arrange a climb up Mount Hanang is through Bush Routes Adventures, which also offers an excellent four-day trip combining an ascent with a visit to a Barbaig community.

Katesh Route
The shortest and most popular ascent is the Katesh route, from Katesh up the southwestern ridge: five to six hours to the summit, camping at 3000m, and a three-to four-hour descent the following day. You can go up and down in one day if the physical challenge is more important than enjoyment, but do start early. Allow time to arrange transport from Babati to Katesh, and to pay the forest fee, so count on a minimum of two or three days in total.

Gendabi Route
To vary the scenery, descending via the Ngendabi route is recommended, or alternatively ascending along it and descending to Katesh. The route starts 16km (3hr) northwest from Katesh at Ngendabi village, Accommodation in Ngendabi offered informally by teachers from the primary school, but shouldn't be counted on.

Giting Route
The main alternative to the Katesh and Ngendabi routes is the Giting route, from Giting village on the northeast side of the mountain. You might need your own 4WD of the bad road, You'll also need to visit Katesh first to pay the forest fee. Accommodation along this route has been planned for years, to take advantage of the beautiful view of Lake Balangida; enquire whether this has finally happened in Babati.

Camping is possible on all routes, but you need to be fully self-sufficient; take enough water as there's none near the summit and no guarantee of any further down. Don't underestimate the mountain: it gets pretty cold at 3417m so come suitably equipped.

 

SOURCE: http://www.bushroutes.com/Tanzania/Mountains/hanang-mountain.html

Thursday 29 May 2014

KUHUSU HANANG


Ramani ya mkoa wa Manyara
Hanang ni moja kati ya wilaya tano zilizopo katika mkoa wa manyara nchini Tanzania. Ipo umbali wa kilomita 242 kusini magharibi mwa Arusha, na km 197 kwa kipimo cha anga (Flight Distance). Kwa upande wa kaskazini imepakana na wilaya ya Mbulu na Babati, kusini mashariki ni mkoa wa Dodoma, na kusini magharibi ni mkoa wa Singida. Kulingana na sensa ya mwaka 2012 wilaya ya hanang ilikuwa na jumla ya watu 275,990.

Wilaya ya hanang imegawanywa katika kata 25 ambazo ni:

·   Balangdalalu
  • Bassodesh
  • Bassotu
  • Dirma
  • Endasak
  • Endasiwold
  • Ganana
  • Gehandu
  • Gendabi
  • Getanuwas
  • Gidahababieg
  • Gisambalang
  • Gitting
  • Hidet
  • Hirbadaw
  • Katesh
  • Lalaji
  • Laghanga
  • Masakta
  • Masqaroda
  • Measkron
  • Mogitu
  • Nangwa
  • Simbay na
  • Sirop

Watu na style za maisha
Ramani ya Wilaya ya Hanang

Wilaya ya Hanang imekaliwa na makabila makubwa mawili ambayo ni Wairaqw na Wabarbaig. Wabarabaig wamekuwa kivutio kikubwa sana cha watalii wa nje kutokana na tamaduni zao ambazo hazijaathiriwa sana na tamaduni za kimagharibi. Wageni wamekuwa wakivutiwa sana na mavazi ya asili ya ngozi kwa wanawake na mashuka mekundu maarufu kama migorori iliyotengenezwa kwa ustadi wa hali ya juu na kupambwa na shanga za rangi mbambali na vifungo vilivyoshonwa kwa ufundi na kuwekwa marinda maarufu kama “sapsapt”

Wageni wako huru kujichanganya na makabila haya na kupokelewa kwa ukarimu kama ilivyo asili ya makabila haya.


Kama unapeda ndege Hanang ndo sehemu ya kuwaona kwani kuna zaidi spishi 400 za ndege watakaokusindikiza kwa nyimbo kipindi chote utakapokua unatembelea maeneo tofauti ya wilaya hii. 

Wednesday 28 May 2014

ZIARA YA KATIBU MKUU WA CHAMA CHA MAPINDUZI TAIFA NDUGU ABRAHAMAN KINANA KATIKA ZIARA YAKE WILAYANI HANANG’ TAREHE 27/5/2014.


Katika kuhakikisha kuwa ahadi zote za chama cha mapinduzi zinatekelezwa kama zilivyoahidiwa katika ilani ya uchaguzi mwaka 2010, katibu mkuu wa chama cha mapinduzi Ndg. Abrahaman Kinana amezuru wilaya ya Hanang’ tarehe 27th May 2014, ikiwa ni siku ya kwanza ya ziara yake ya siku saba mkoani Manyara. Katibu mkuu ameongozana katibu mwenezi wa CCM kijana machachari Nape Nauye, Mbunge wa Hanang’ na waziri wa uwekezaji na uwezeshwaji Mhe. Mary Nagu, Waziri mkuu wa zamani Mhe. Fredrick Sumaye na makada wengine wa Chama cha Mapindzi.

Akihutubia katika viwanja vya chama cha mapinduzi vilivyokuwa vimefurika watu hadi kukosa sehemu ya kusimama Ndg. Kinana aliwataka wananchi wa wilaya ya Hanang kuacha kupiga zogo za kisiasa na kufanya shughuli za maendeleo zitakazowaingizia kipato.

Akizungumza kwa msisitizo Ndg. Kinana aliwataka wananchi kuunga mkono juhudi za serikali katika kuleta maendeleo kwa kutokataa kutoa michango muhimu akitolea mfano mchango wa kujenga maabara katika shule za sekondari, na ujenzi wa hospitali, pia aliwataka wafanyabiashara kukaa na madiwani wao kama wanaona kodi ni kubwa ili wapunguziwe kwani madiwani wengi sio wafanyabiashara hivyo hawajui tamu na chungu ya biashara.

Aidha kuhusu migogoro ya ardhi ikiwemo Mashamba ya NAFCO ngd. Kinana aliahidi kuwa wawekezaji wote wanaokodisha mashamba hayo watachukuliwa kama wameshindwa kuyaendeleza na watanyang’anywa na kurudishwa kwa wananchi. Pia alisisitiza kuwa sio azma ya serikal kumpa mwekezaji moja mkubwa ili yeye awakodishie watu wengine kidogokidogo, mbunge wa wilaya Hanang’ alimuunga mkono kwa hilo kwa kusisitiza kuwa wawekezaji wote wanaokodisha mashamba hayo watanyang’anywa na kurudishwa kwa wananchi.

Na mwisho kuhusu katiba mpya Ndg. Kinana alisema muundo wa serikali hauleti vyakula mezani mwetu wala fedha mifukoni mwetu na kusisitiza kuwa CHADEMA wanataka serikali tatu kwa uchu wa madaraka tu na sio kwa kuwatakia mema watanzania, Ndg. Kinana alisisitiza kuwa chadema wanaamini kuwa zikiundwa serikali tatu, wao watashinda bara, CUF watashinda Zanzibar na CCM watachukua serikali ya tatu ya shirikisho. Aidha ndugu kinana alisema kuwa katika bunge la katiba tumeshuhudia kigeugeu cha chadema wakitaka mara kura ya wazi, mara siri, na pia kwa kipindi chote wamekuwa wakizungumzia mgawanyo wa madaraka badala ya kero za wananchi. Akiendelea kutolea ufafanuzi ndg. Kinana alisema katiba ya Tanzania imefanyiwa marekebisho mara 14 kwa kipindi cha miaka 50 tangu tupate uhuru, lakini katiba ya marekani imefanyiwa marekebisho mara saba tu kwa muda wa zaidi ya miaka 280. <swali> Je, katiba yetu ni bora kuliko ya marekani au ni kama nguo iliyochakaa kwa kupigwa viraka kila sehemu?

Baada ya hotuba nzuri ya Ngd. Kinana ailgawa mizinga 140 kwa vikundi kumi vya ujasiriamali na pia kugawa kadi kwa wana wapotevu waliorudi kundini kwa kurudisha kadi za chadema na kuchukua kadi zao mpya za CCM.

Monday 17 March 2014

The Origin of Hanang Vijana SACCOS

Katika kuttekeleza sera ya Chama Cha Mapinduzi, Mkuu wa wilaya ya Hanang
Mh. Christina Mndeme, aliwakutanisha vijana kutoka kata zote za wilaya ya Hanang, na baada ya kujadili changamoto za kimaisha zinazowakabili vijana hao kwa pamoja walikubaliana kuanzisha SACCOS ambayo itakuwa chombo cha kuwaunganisha vijana hao na kutoa mikopo yenye masharti nafuu, itakayowawezesha vijana hao kujikomboa kiuchumi.
Mkuu wa wilaya ya Hanang Mhe. Christina Mndeme.


Akizungumza na gazeti hili mkuu wa wilaya ya Hanang alisema Shirika hili lilianzishwa kwa lengo la kuwakwamua vijana kichumi na kupanua wigo wa ajira kwa vijana na kuamsha vipaji na uwezo wao wa kufanya kazi kwa kuunda vikundi vidogovidogo vya wajasiriamali na kuwapa elimu na mikopo yenye masharti nafuu itakayowawezesha vijana kujipatia kipato na kuwa chachu ya maendeleo yao, jamii inayowazunguka na Wilaya kwa ujumla
Akitolea ufafanuzi mkuu wa wilaya ya Hanang alisema wameanzisha vikundi vitano ambavyo ni kikundi cha wafuga nyuki, waendesha bodaboda, kilimo, wafugaji wa kuku wa kienyeji na kikundi cha wafyatua matofali ya kisasa kwa technolojia ya hydroform,

Taskforce ya Hanang Vijana Saccos

Akaindelea kufafanua mkuu wa wilaya ya Hanang alisema “Shirika hili lilianzishwa chini ya sheria ya vyama vya ushirika na 20 ya mwaka 2003, na kanuni za vyama vya ushirika za mwaka 2004, na kusajiliwa tarehe 04/12/2013 kwa nambari ya usajili MNR/144 Ikiwa na wanachama waanzilishi 316, na sasa tunajivunia kuwa na wanachama hai zaidi ya 400 na bado tunawahamasisha wote wa kike na wa kiume waishio wilaya ya Hanang wenye umri kati ya miaka 15 na 35 wajiunge na Saccos hii”

Aidha mwenyekiti wa kamati ya mpito ya SACCOS hiyo Bw. Dominick Duncan alisema kuwa “Hii inaonesha nia ya dhati ya serikali katika kutokomeza umasikini, na kuwakomboa vijana ambao ndio nguvu kazi ya taifa” akaongeza “Vijana wengi tulikuwa hatuna ajira rasmi, hivyo hatukuwa na kipato cha uhakika, hii ilitupelekea vijana wengi kukosa matumaini na kujiona kama kundi lililosahaulika katika jamii, lakini SACCOS hii imefufua matumaini yetu, na leo najivunia kuwa kijana wa kitanzania” 

Thursday 27 February 2014

Tangazo

Ndugu wajumbe wa Hanang Vijana Saccos, tunasikitika kuwatangazia kuwa uzinduzi wa saccos yetu umeahirishwa mpaka hapo tutakapopewa taarifa rasmi. Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

Tuesday 25 February 2014

TANGAZO

VIJANA WOTE WA WILAYA YA HANANG, MNAKARIBISHWA KWENYE UZINDUZI WA SACCOS YA VIJANA WA HANANG SIKU YA TAREHE 01/03/2014 KATIKA VIWANJA VYA SHULE YA MSINGI KATESH, KUANZIA SAA TATU KAMILI ASUBUHI (9:00AM), MGENI RASMI ATAKUWA WAZIRI WA VIJANA UTAMADUNI NA MICHEZO Mhe. Dk. FENELLA MUKANGARA, WAZIRI WA UWEZESHWAJI NA UWEKEZAJI NA MBUNGE WA HANANG Mhe. Dk. MARY NAGU, NA PIA WAGENI WAALIKWA KUTOKA NATIONAL HOUSING CORPORATION (NHC), BARAZA LA UWEKEZAJI NA UWEZESHAJI TANZANIA VIONGOZI WA WILAYA, MKOA NA VIONGOZI WENGINE WA KITAIFA.
VIJANA WOTE MNAKARIBISHWA KATIKA UZINDUZI HUO. 
 
KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NA:
M/KITI WA TASKFORCE: DOMINICK DUNCAN
AU WAFIKE OFISI YA VYAMA VYA USHIRIKA: KILIMO KATESH.
AU PIGA SIMU NO.
0766988891
0786230675

Wednesday 19 February 2014

TANGAZO

Wajumbe wa HANANG VIJANA SACCOS, nasikitika kuwataarifu kuwa kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wetu, Uchaguzi  umehairishwa mpaka hapo mtakapopewa taarifa zaidi. Samahani kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.